Mbwana Ally Samatta (alizaliwa 23 Disemba 1992) jijini Dar es salaam ni mchezaji wa mpira wa miguu wa Tanzania anayecheza nafasi ya mshambuliaji katika klabu ya K.R.C Genk nchini Ubelgiji na nahodha wa timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars.![](https://scontent.fmba3-1.fna.fbcdn.net/v/t1.0-9/71667986_108893430521874_1108202408200110080_n.jpg?_nc_cat=108&_nc_ohc=o5mBO44dtqcAQm6paRdcQjh_spcmKHhtaOaK3HkIekRWZOyc94vkEYPQQ&_nc_ht=scontent.fmba3-1.fna&oh=55ad9b446853c33020c1e9878e4703f4&oe=5EA211A1)
![](https://scontent.fmba3-1.fna.fbcdn.net/v/t1.0-9/71667986_108893430521874_1108202408200110080_n.jpg?_nc_cat=108&_nc_ohc=o5mBO44dtqcAQm6paRdcQjh_spcmKHhtaOaK3HkIekRWZOyc94vkEYPQQ&_nc_ht=scontent.fmba3-1.fna&oh=55ad9b446853c33020c1e9878e4703f4&oe=5EA211A1)
Samatta alianza kucheza soka la kulipwa katika klabu ya African
Lyon mwaka 2008 Ya nchini Tanzania. Alisajiliwa na klabu ya Simba S.C. mwaka 2010, ambapo alicheza kwa nusu
msimu tu kabla ya kujiunga na klabu ya TP Mazembe kutokea DRC, alicheza kwa miaka mitano ndani ya TP
Mazembe na kujijengea nafasi katika kikosi cha kwanza cha klabu hiyo. Mwaka
2015, alishinda taji la mcheza bora wa mwaka wa Afrika, na kumaliza msimu akiwa
mfungaji bora wa mashindano ya klabu bingwa Afrika (CAF Champions Ligi) na
kuisaidia klabu yake kshinda taji hilo.
Samatta alijiunga na klabu ya KRC Genk ya nchini Ubelgiji manamo
januari 2016, aliisaidia kufuzu michuano ya Ulaya maarufu kama Europa Ligi na
kushinda taji la ligi ya Ubelgiji (Belgian
Jupiler Ligi mwaka
2019. Alimaliza msimu akiwa mfungaji bora wa ligi ya Ubelgiji na akashinda tuzo
ya mchezaji bora wa ligi ya ubelgiji (Ebony Shoe
award).
Samatta alikua mchezaji muhimu wa TP Mazembe waliposhinda taji la klabu bingwa Afrika
mwaka 2015 (2015
CAF Champions Ligi), akifunga jumla ya magoli saba na kumaliza akiwa mfungaji
bora.[1]
Mnamo Januari 2016, aliposhinda tuzo ya mchezaji bora wa Afrika,
aliweka rekodi ya kuwa mchezaji wa kwanza kutokea Afrika ya Mashariki kutwaa
tuzo hiyo. Katika ugawaji wa tuzo hizo uliofanyika jijini Abuja Nigeria tarehe
7 Januari 2016, Samatta alikusanya jumla ya alama 127, akimzidi mchezaji
mwenzake Robert
Kidiaba mlinda lango wa
TP Mazembe na timu ya taifa ya DR Congo aliyepata alama 88. Baghdad
Bounedjah raia wa Algeria
alishika nafasi ya tatu akiwa na alama 63.[2]
Katika mchezo dhidi ya Moghreb
Tétouan ya Moroko,
Samatta alifunga goli tatu kwa mpigo (hat-trick) iliyowafanya wasonge hatua ya
nusu fainali ya klabu bingwa Afrika, magoli hayo yanakumbukwa sana katika
historia ya klabu ya TP Mazembe.[3]
Muda mfupi baada ya kushinda tuzo ya mchezaji bora wa Afrika,
aljiunga na klabu ya K.R.C Genk kwa mkataba wa miaka minne na nusu.[4] Tarehe 23 Agosti 2018 Samatta alifunga goli tatu kwa
mpigo(hat-trick) dhidi ya Brøndby IFkwenye mashindano ya Ulaya maarufu kwa jina
la Europa Ligi walfanikiwa kupata ushindi wa goli 5–2.[5]
Mbwana samatta ameweka rekodi ya kuwa
mtanzania pekee aliecheza michuano ya Uefa champions ligue licha ya timu yake kutokufanya vizuri katika mashindano hayo, na alifanikiwa kufunga mabao
matatu katika michezo 6, historia pekee nay a kukumbukwa ni pale alipoifunga
Liverpool nyumbani Anfield…………INSERTS
Mbwana Samatta wakati akiichezea simba alifunga mabao 13 katika
michezo 25, na baadae Tp mazembe alifunga mabao 60 katika michezo 103, mpaka
sasa Samatta ameichezea Genk michezo 98 na kufunga mabao 43, na timu ya taifa
ya Tanzania michezo 56 mabao 20, jumla akifunga mabao 136 katika michezo 282.
mpaka sasa ameshinda tuzo mbalimbali ikiwemo
ubingwa wa ubelgiji, supa cup ubelgij, ubingwa
wa Tp mazembe vikombe 7, mchezaji bora wa bara la afrika, mchezaji bora wa
ubelgij kwa wachezaji wenye asiri ya bara la afrika.
Mbwana samatta amemuoa mrembo Neima Mgange na
kufunga nae ndoa jijini dar es salaam. Mbwana samatta ni mdogo wa mchezaji wa
Kmc Mohamed Samatta ambao wote wametokea katika familia yam zee Alli Samata
mchezaji wa zamani wa Balimi fc.
Nikukumbushe tuu Baba yake mbwana samatta
alimpata mama samatta wakati akiwa mchezaji wa balimi fc huko mkoani kagera na
mama yake samatta alikuwa askari ambae kabla ya hapo mama yake samatta alitoa
ofa kwa mchezaji atakae funga bao atapata zawadi ya soda ndipo mzee Samatta
alipofunga bao na kwenda kuchukua zawadi yake na hapo mahusiano yao yalipoanza
chanzo kikiwa ni soda. hahahahaa
🎉 Happy
Birthday, Mbwana Samatta
Makala hii imeandaliwa na Alex Mwenda Daady
No comments:
Post a Comment