Miraj
Athuman Madenge Sheva winga wa kimataifa wa Tanzania na klabu ya simba,
alizaliwa desember 27 1993 jijini Dar es salaam katika familia ya mzee Madenge.![Taswira inaweza kujumuisha: Mtu 1, kusimama, viatu, mtoto na nje](https://scontent.fmba3-1.fna.fbcdn.net/v/t1.0-9/78108518_501029200504187_1677835438108180480_n.jpg?_nc_cat=100&_nc_ohc=4tqPKXqZZ5sAQm0xF6CT4ida3luBIy2k0sUHS_mL5Tm_pwx6A3pHgfQJg&_nc_ht=scontent.fmba3-1.fna&oh=3f8a32468713729477e7e9f60349c304&oe=5E6E3B9C)
![Taswira inaweza kujumuisha: Mtu 1, kusimama, viatu, mtoto na nje](https://scontent.fmba3-1.fna.fbcdn.net/v/t1.0-9/78108518_501029200504187_1677835438108180480_n.jpg?_nc_cat=100&_nc_ohc=4tqPKXqZZ5sAQm0xF6CT4ida3luBIy2k0sUHS_mL5Tm_pwx6A3pHgfQJg&_nc_ht=scontent.fmba3-1.fna&oh=3f8a32468713729477e7e9f60349c304&oe=5E6E3B9C)
Alianza
kujihusisha na masuala ya soka wakati akiwa shule ya msingi na sekondari ambao
rasmi aliingia katika soka na kuitumikia timu ya Sifa united yenye maskani yake
jijini Dar es saalam.
Baada ya
kuonesha uwezo mzuri akasajiliwa na simba B ambapo pia hakudumu klabuni hapo na
kuamua kutafuta maisha sehemu nyingi alipotimkia Toto afrika ya mwanza mwaka
2015.
Baada ya
msimu mzuri klabuni hapo akatimkia Afrika lyon ambapo napo hakudumu sana, baada
ya timu hiyo kushuka daraja nae alitimka klabuni hapo.
Alionesha
uwezo mzuri wa kufumania nyavu licha ya kikosi hicho kuonekana dhaifu ndio
Simba walipomtwaa kwa mara nyingine. Hakupata nafasi katika kikosi cha wakubwa
na kuamua kutimkia Mwadui fc ya mkoani Shinyanga ambapo kule nako aliuwasha
moto kiasi cha kuvitoa udenda vilabu vya simba na yanga.
Msimu wa
mwaka 2018]2019 aliamua kwenda kujiunga na Lipuli fc ya mkoani Iringa ambapo
alionesha uwezo mkubwa wa kufumania nyavu na kuvitamanisha tena vilabu vikubwa,
alitengeneza safu bora ya ushambuliaji ndani ya Lipuli ikiongozwa na Paul
Nonga, Haruna shamte, daluesh saliboko pamoja na jimmy shoji mwaisondola, na
kuiwezesha Lipuli fc kucheza fainali ya FA na kupoteza dhidi ya Azam fc.
Alex Mwenda
Daady ambae ni mwaandaaji wa Makala hii anaendelea kumwangazia Miraji Athuman
ambae alisajiliwa simba kimya kimya bila mbwembwe zozote zile.
Alionekana
katika mchezo wa kwanza wa kirafiki wa Simba vs Gwambina fc akivaa uzi mwekundu
ndipo alipozua maneno kwa mashabiki wakihofia uzoefu wake kama atakuwa sehemu
ya kikosi cha Simba.
Na hatimane
Simba day jina La miraji Athumani likatajwa.
Baada ya
kutua klabu hapo ndipo moto ulipoanza kuwaka kwa upande wake, mechi ya kwanza
dhidi ya Jkt tz akitokea benchi alifunga bao la tatu assint saf ya meddie
kagere, simba ikisha bao 3-1.
Katika
mchezo wa pili akitoa benchi tena ndie aliekwenda kufunga bao la ushindi vs
Mtibwa sugar simba ikiibuka na ushindi wa magoli 2-1.
Hapo ndipo
moto wake rasmi ulipowaka akicheza mechi dhdi ya kagera licha ya kutofunga
aliiisadia timu kutengeneza bao baada ya kuangushwa ndani ya 18.
Na akazidi
kufunga na kufunga. Miraj Athuman sheva ndie mchezaji bora wa ligi kuu nchini
kwa mwezi September, alipowashinda meddie kagere na ismail kada wa tz prisons.
Happy
birthday Miraj Athuman Madenge aka Sheva kwa kutimiza miaka 26 hii leo.
Makala hii
imeandaliwa na Alex Mwenda Daady
No comments:
Post a Comment