MAYWEATHER
Imeandaliwa na Alex Mwenda-Songea
Wazazi wengi huwasisitiza vijana wao wasome ili
waje kuwa na maisha bora hapo baadae huku imani ikiwatuma kusoma ndio mtaji
mzuri wa maisha hapo baadae. Hapa Tanzania siasa ndo kitu chenye kuleta manufaa
zaidi. Lakini kwa shujaa wetu wa hii leo mambo ni tofauti hajui kusoma wala
kuandika ila ngumi yake ikitua kichwani inaondoka na ubongo na ndie tajiri
zaidi duniani kwa upande wa mapambano.
Jina lake halisi anaitwa Floyd
Joy Sinclair lakini wengi wanamfahamu kwa jina la Floyd Myweather alizaliwa Februari 24, 1977 huko Grand
Rapid, Michigan nchini Marekani
kutoka kwa mama, Deborah Sinclair na
baba yake Floyd Mayweather Sir.
Ana urefu wa futi 5 na nchi 8 na uzito wa kilo 68.5, akiwa
ni bondia mwenye rekodi ya aina yake katika masumbwi ya uzito wa Middle
Weight na Super Feather Weight.
Mpaka sasa ameshashiriki mapambano 50, hajapoteza pambano
hata moja, na kati ya hayo, 27 ameshinda kwa ‘knock out’, huku akitwaa mikanda
15 ya ngazi ya dunia, mitano kati ya hiyo akiishikilia kwa miaka minne
mfululizo.
Mayweather ameingia
katika rekodi ya mabondia wanaolipwa mshahara mkubwa zaidi kwa mwaka, pambano
lake la mwaka 2015, alilipwa bilioni16.5 kapambana na Man Pacq-yao, alimpiga
bondia kutoka Ufilipino, Manny Pacquiao mwenye urefu wa
futi tano na nchi 5, na uzito kilo 66, baada ya kuibuka mshindi katika pambano
hilo mashabiki walimpachika jina la The Best Ever.
Mayweather anamiliki jeti au
ndege binafisi aina ya GulfStream GV aliyoinunua
kwa gharama ya Sh4.2 bilioni. Ndege hiyo ina uwezo wa kuwabeba abiria 18, ambao
huwa wanaunda timu yake ya 'The Money Team’.
Aidha Boksa huyu ana magari ya kutosha zaidi zikiwa za kifahari na zenye bei ya juu. Mayweather ana
zaidi ya magari 10 yenye bei mbaya. Kutokana na idadi kubwa ya magari
aliyonayo, amezitengea mitaa mbalimbali ya kutanua nazo.
Kuna zile za Las Vegas Collection
anakoishi ambazo zote ni za ragi nyeupe, kuna zile za Miami Collection
anakopenda kwenda kujivinjari ambazo zote ni za rangi nyeusi, kuna pia Los
Angeles Collection na zingine kibao.
Gari lake la kwanza alilinunua akiwa na
umri wa miaka 19 1996 Mercedes Benz shilingi za kitanzania milioni
600 ambayo anamiliki hadi leo. Ila kati ya zile
anazopenda sana ni Bugatti zake tatu ambazo alinunua kila moja kwa kitita cha
Sh203 milioni.
Bondia huyu anamiliki majumba kadhaa
anazokodisha katika miji ya New York, Los Angeles, Las Vegas na Miami. Mwaka
jana aliuza mojawepo ya majumba yake inayopatikana Miami kwa kitita cha Sh238
milioni. Makao yake yanapatikana Las Vegas anakoishi kwenye jumba la thamani ya
Sh824 milioni
Kila
anapoona saa iliyomvutia lazima atainunua kwa gharama yeyote ile. Anamiliki saa
zadi ya 20 zenye bei mbaya, zinazozidi hata kodi ya nyumba. Kati ya saa hizo
adimu kuna aina ya Piaget Galaxy aliyonunua kwa kima cha Sh91.5 milioni,
Audemar Piguet Royal Oak Sh119 milioni na Jacob & Co. Rainbow Tourbillon
Sh183 milioni
Hivi majuzi Mayweather alitangaza
kuwa hutumia kiasi cha Sh400,0000 kununua
chakula chake cha kila siku. Aidha anatumia
kitita kingine cha Sh25 milioni kumlipa
mpishi mmoja kwa jina Chef Q anayehusika kumwandalia mlo kwa
mwaka. Aidha mpishi huyo Chef Q anadai kuwa hatozi
kiasi hicho kikubwa cha fedha kwa mapishi yake ila ni Mayweather ndiye
aliyemsisitizia malipo hayo ambayo kwa sasa Chef Q Ndie mpishi wa
ndani tajiri zaidi duniani akiwa na utajiri wa bilioni 8 sawa kabisa Diamond
platnumz.
Myweather bado ni mtu ambae kila kila kwake ni hela hela tu mwaka
2015 Alipokuwa akitia sahihi mkataba wake wa pigano
dhidi ya Manny paqyao, Floyd alitumia
kalamu ya dhahabu kwa jina 'Peerless’ yenye thamani ya Sh366,000. Kalamu hiyo
ilitengenezwa na vipande 18 vya dhahabu.
Kalamu hiyo inamilikiwa na watu 124 pekee
kote duniani akiwemo aliekuwa Rais wa
zamani wa Marekani Barrack Obama na mtangazaji mashuhuri
na mwanamke mweusi tajiri zaidi duniani Oprah Winfrey.
Kila mwaka Mayweather hutumia kiasi cha
Sh549,000 kununua nguo zake za ndani pekee na kila anapovaa hazirudii tena yeye
huzivua na kuzitupa. Viatu vile vile havai mara mbili hata anapokuwa kwenye
ziara za nje, anapoondoka hoteli yeye huviacha kwa wahudumu wa hotelini.
FAMILIA ya Floyd Mayweather kwa hapa nyumbani unaweza
kuifananisha kabisa na ile ya Matumla, iliyojaa mabondia wengi wenye vipaji
kuanzia babu, baba hadi wajukuu na ikiwezekana hata kina dada.
Mayweather Jr ndiye bondia mwenye uwezo mkubwa kuliko wengine
wote hadi sasa kwa kuwa hajapigwa hata pambano moja. kwa KO.
Mayweather ni bilionea ambaye utajiri wake sasa unafikia dola
milioni 500 alizopata kupitia mchezo wa ngumi na hasa za kulipwa kabla ya
pambano la jana alfajiri. Lakini mkali huyo anayetokea Las Vegas, Nevada nchini
Marekani amewekeza kwenye maisha ya kifahari zaidi.
Ni kati ya wanandondi wenye urafiki mkubwa na wasanii mbalimbali
wa muziki na waigizaji kutoka Hollywood nchini Marekani.
Kwa sasa Justin Beiber na Lil Wayne ndiyo watu wake wa karibu
zaidi. Awali alikuwa rafiki wa karibu wa 50 Cent lakini ilielezwa walitibuana
sababu ya kugombea mwanamke na 50 cent ndiye alishikwa kwa usaliti.
Pamoja na utajiri wake mkubwa, Mayweather amekuwa akisisitiza
kwamba kamwe maisha yake hayajawa rahisi kama watu wengi wanavyofikiri na mara
nyingi amemlaumu baba yake mzazi, Mayweather Sr hadharani kuwa amekuwa tatizo.
Mayweather amewahi kutumia madawa ya kulevya kama ilivyo kwa
mama yake na baba yake pia ambaye alikuwa muuzaji mkubwa na amekuwa akikubali
kweli aliuza kwa lengo la kuisaidia familia yake na hata Mayweather alikuwa
akipata fungu lake.
Bondia huyu ambaye pia ni mjasiriamali ana miliki akaunti
moja ya benki yenye zaidi ya dola milioni 600 ndani yake, na hakuna anaeijua
nambari ya siri ya account yake ya mabilioni hayo zaidi ya bibi yake ambae ndie
aliegundua kipaji chake cha mapigano, na kwa sasa bibi huyo ni marehemu.
Mayweather ni
kiongozi wa kundi liitwalo The Money Team (T.M.T), na
upande wa pili wa maisha ya kimapenzi, bado hajaoa hadi sasa ila ni baba
wa watoto wanne kwa wanawake tofauti, mpenzi wake wa awali Jossie
Harris amezaa naye watoto wawili wa kiume Koraun na Zion,
na mmoja wa kike anayeitwa Jirah.
Mtoto wake wa mwisho anaitwa Iyyana, amezaa
na mpenzi wake mwingine, Mellisia Brim. Alishawahi kutumikia
kifungo jela huko Las Vegas kwa kosa la
unyanyasaji na vurugu.
Tangu mwaka 1996 ameshinda tuzo 30 bora zaidi
duniani. Baba yake pia wa froyd alikuwa mpigaji na alipambana mapambano 35
akishinda 28 akipoteza
No comments:
Post a Comment