![Image result for mrisho ngasa](https://mobile.mwanaspoti.co.tz/image/view/-/2509836/lowRes/867023/-/gxalje/-/ngassa_clip.jpg?format=xhtml)
Imeandaliwa na Alex Mwenda...........watsap 0759-238235
MRISHO
NGASSA
Shujaa wa keysports leo tunamwangazia mtanzania aliepata
mafanikio makubwa katika soka la nchii hii ya Tanzania, kama ambavyo mwandishi
wa makala hii Alex mwenda daady anamwangazia.
Jina lake ni Mrisho Ngassa (amezaliwa 5 Mei 1989)
ni mchezaji wa mpira wa miguu kutoka Tanzaniaambaye anaichezea klabu mashuhuri
Tanzania Young Africans FC
Alianza maisha yake ya soka huko jijini mwanza katika timu za
madaraja ya chini klaba ya kupandishwa kuichezea Toto afrikan wanakisha mapanda
wa mwanza, kutokana na uwezo wake kuwa mkubwa hakudumu klabuni hapo na kisha kutimkia
mkoani kagera kwa timu ya kagera sugar wanankurukumbi mwaka 2005-2006.
Nakumbuka
vizuri, Mrisho Ngassa alichomolewa kutoka mafichoni huko kwenye timu ya Geita
Gold Mine na kocha aliyemfahamu siku nyingi, Sylvestre Marsh na kumpeleka
Kagera Sugar timu aliyokuwa akiifundisha na kuipatia mafanikio, huko ndiko
Ngassa alikoanza kujulikana.
Ngassa
angeweza kuwa amejulikana kama angepata nafasi ya kucheza kwenye timu ya Taifa
ya vijana chini ya miaka 17 ‘Serengeti Boys’ iliyokuwa chini ya kocha Abdallah
Kibadeni lakini hakubahatika kupata nafasi ya kucheza licha ya kuwemo kwenye
timu hii, labda ilichangiwa na umbo lake lilivyokuwa dogo zaidi badala yake
alianza kujulikana alipofanya vizuri kwenye Ligi Kuu Bara 2006 akiwa na Kagera
Sugar ingawa mashindano yaliyomtoa yalikuwa ni yale ya Tusker mwaka 2006
yaliyofanyika Dar es Salaam hasa baada ya timu ya Kagera Sugar kuwafunga Simba
2-1 kwenye wa fainali.
Baada
ya mashindano hayo Simba walikuwa wa kwanza kutangaza nia ya kumsajili Ngassa
tena kwa kitita cha Sh 1 milioni lakini kwa mshangao wa wengi Ngassa aliwaita
Yanga kwa kusema ‘Yanga njooni upesi kunisajili’ Yanga waliitikia wito na huo
ukawa mwanzo wa Ngassa kutua Yanga.
Baada
ya kutua Yanga, Ngassa alianza kuisaidia kupata mafanikio, baada ya kuukosa
ubingwa wa Bara kupitia iliyoitwa ligi ndogo ya kubadili msimu mwaka huohuo
mjini Morogoro, mwaka uliofuata Ngassa akisaidiana na wenzake waliipa Yanga
ubingwa, huo ulikuwa mwanzo mzuri kwake kuwika Yanga na kuanza kuwa mchezaji
tegemeo kwa muda wote huo licha ya kelele za wapenzi wa soka kutaka kocha wa
Taifa Stars wakati huo, Marcio Maximo amwite kwenye timu ya Taifa, yeye
alifumba macho akimtaka Ngassa aongeze bidii.
Haikuchukua
muda mrefu, Maximo alimwita kwenye kikosi chake mwishoni mwa mwaka 2008,
alifanikiwa kumbadilisha kiuchezaji kutoka kwenye ukimbiaji wa pembeni zaidi,
hadi kucheza kwa malengo zaidi na akafanikiwa kumfanya kuwa mshambuliaji badala
ya winga.
Msimu
wa mwaka 2009 ulikuwa wa mafanikio zaidi kwa Ngassa, ambaye aling’ara vizuri
akiwa na Yanga na timu za Taifa, hali hiyo ilimfanya kuanza kuutambua uwezo na
mchango wake Yanga akilinganisha kipato chake (mshahara) mbele ya wachezaji
wengi anaowazidi uwezo hasa wa nje kama Ben Mwalala, Jonh Njoroge na wengineo.
Hatimaye aliamua kuanza mazungumzo na uongozi
wa Yanga akiomba aboreshewe mkataba wake kwa kuongezewa mshahara, lakini
uongozi chini ya Mwenyekiti Iman Madega ulipuuzia, hawakuuthamini mchango wake
na ndipo Azam walipopata nafasi ya kufanya mazungumzo naye na kumsajili kuanzia
msimu wa 2010/2011.
Hakuwa
na msimu mzuri ndani ya Azam fc ambako nako walimtoa kwa mkopo kuelekea Simba
sc mwaka 2012-2013 baada ya mkopo wake kumalizika alifanya maamuzi ya kurejea
tena Yanga.
Kati ya
mambo yanayonishangaza na hata kuwashangaza wachezaji wengi wa sasa na wale wa
zamani ni jinsi Ngassa anavyojitofautisha na wachezaji wengine kwa kuonyesha
mapenzi ya dhati Yanga, achilia mbali Ngassa kuibusu nembo ya jezi ya Yanga
akiwa Azam na kuendelea kuwapungia mikono mashabiki wa Yanga alipokuwa Azam,
Simba au akiwa Taifa Stars.
Mambo
aliyojitofautisha na wachezaji wa zamani au hata wa leo ambao kwa nyakati
tofauti wamezichezea Simba na Yanga kina Edibily Lunyamila, Mohammed Hussein,
Ali Yussuf Tigana, Zamoyoni Mogella, Athumani China, Mwanamtwa Kihwelu, Omary
Hussein, Godwin Aswile, Hamis Gaga, Method Mogela, Said Mwamba na wengineo hawakuwahi
kuonyesha hadharani mapenzi ya dhati kwa timu waliyoipenda kama Ngassa.
Ilikuwa
kawaida kwa Ngassa alipohamia Azam kumuona akiwa na bukta ya Yanga kabla ya
kuvaa nguo za mazoezi za Azam, ni kawaida kwake kukaa katika upande wa
mashabiki wa Yanga inapocheza michezo ya kimataifa au kirafiki na timu za nje
siku ambayo Azam au Simba walikuwa mapumzikoni.
Hii
inakuwa ni kielelezo cha mchezaji kuwa na mapenzi ya dhati kwa timu fulani
hivyo sioni sababu ya timu nyingine kumuhangaikia.
Ngassa
ni ‘Profesheno’
Ngassa
amejitofautisha kimtazamo nje na ndani ya timu alizokuwa anazichezea za Azam na
Simba, aliwahi kusema Kocha wa Simba Patrick Liewig kwamba ‘wachezaji wanapaswa
kuiga uchezaji wa kujituma wa Ngassa ambaye aliijua na kuithamini kazi yake,
alikuwa na nidhamu ya mazoezi na hata kambini.
Katika
msimu wake wa kwanza tu akiwa Azam aliisaidia kushika nafasi ya tatu na yeye
kuwa mfungaji bora msimu wa 2010/11 kwa mabao yake 16. Usingeweza kumtofautisha
Ngassa wa Azam na Ngassa wa Yanga, tofauti ilikuwa ni majukumu na nafasi
aliyopewa akiwa Azam hasa katika mfumo wa 4:3:3 iliomlazimu Ngassa kushambulia
akitokea pembeni zaidi tofauti na alivyocheza Yanga, alikuwa akicheza kama
mshambuliaji wa pili nyuma ya mshambuliaji wa kati kitu ambacho kilikuwa
kinampa uhuru zaidi.
Angalau
alipofika Simba na hasa baada ya Okwi kuondoka, Ngassa alipewa majukumu ya
kucheza nyuma ya mshambuliaji wa mwisho, hali hiyo ilimfanya kuisaidia zaidi
Simba, alikuwa chachu ya ushindi wa Simba, alitoa pasi nyingi za mwisho ambazo
wachezaji wa Simba walizitumia kufunga.
Ni
profesheno kwa sababu hakuonyesha kuchoka, alipigana sana ili timu yake
ishinde, hakuonyesha mapenzi uwanjani kwani ni kati ya wachezaji ambao
hawapendi kufungwa.
Ngassa
aliushangaza umma wa Watanzania kwa kukataa kujiunga na El-Merreikh ya Sudan
kwa sababu ya kutoshirikishwa katika mchakato mzima wa usajili, wadau wengi
walimlaumu.
Binafsi
nilimuunga mkono kutokwenda Sudan, si kwa sababu hakushirikishwa au sijui
alifichwa na viongozi bali alikuwa sahihi kwa muono wa mbali. Ligi ya
Sudan ni maarufu kwao tu, kwa hiyo isingemsaidia Ngassa kutoka nje.
Baada ya kerejea kwa mara ya pili Yanga, Ngassa alitimkia Afrika
kusini katika klabu ya Free states ambayo ilikuwa ikinolewa na kocha wa zamani
wa timu ya taifa ya Malawi the flames Kinah Phili ambae alikuwa akimhusudu sana
Mrisho Ngassa.
Hakudumu klabuni hapo baada ya kocha kinah phili kufungashiwa
vilago nay eye kutimkia Fanja fc ya nchini Oman, ambako alidumu kwa mwezi mmoja
na nusu klaba ya kuvunja mkataba na kurejea Tanzania. Jambo ambalo watu
waliamini Ngassa analudi tena yanga lakini aliekuwa kocha wa wakati huo
mholanzi Hans del pluijm alikataa kumsajiri na kasha aliamua kuachana na klabu
hiyo.
Baada ya kuona dili lake la kutua Yanga limeshindikana alitimkia
kwa wanakloma kumwantya Mbeya city ambako nako hakudumu kutokana na kudai
stahiki zake na kasha kutimkia Ndanda fc ambako ndiko alifanikiwa kurejesha
kiwango chake ambacho kilimfanya aweze kuludi tena yanga kwa mara ya tatu tangu
mwaka 2006.
Ikumbukwe kuwa Mwezi wa Aprili 2009, Ngassa kutokana na uchezaji
wake mzuri aliweza kumvutia aliekuwa kocha wa wakati huo wa west ham united Francisco Zola klabu ya Uingereza kumualika ili aende kufanya
majaribio ya wiki mbili nakumtizama uwezo wake wa kimpira ili waweze kumnunua,
majaribio yalipoisha West Ham ilizungumzwa kua ni mchezaji mzuri ila anahitaji
baadhi ya vitu fulani navyo ni vya kiufundi katika mambo ya kimpira hata hivyo
inazungumzwa kua kuna baadhi ya klabu barani Ulaya zilipendelea
kumchukua.
Mrisho Ngassa ndie mchezaji pekee nchini alietwaa mataji mengi
zaidi ya ligi kuu Tanzania bara mara 7, kombe la tusker mara mbili.
Mrisho Ngassa alitwaa tuzo ya mchezaji bora wa ligi kuu mwaka
2009-2010. Na mwaka huo huo alitwaa tuzo ya mfungaji bora wa ligi kuu, adiidha
alitwaa tuzo ya mfungaji bora wa CECAFA CUP mwaka 2009, na tuzo kubwa kwake ni
kuwa mfungaji bora wa michuano ya klabu bingwa Afrika mwaka 2013-2014 kwa
kufunga magoli 6.
Alichukua pia tuzo ya mchezaji bora wa mwezi wan ne msimu wa
mwaka 2014-2015.
Mrisho Ngassa ndie mchezaji pekee wa Tanzania aliecheza mechi
nyingi za timu ya taifa mara 100 huku akiwa ndie mfungaji bora wa muda wote
ndani ya timu ya taifa ya Tanzania taifa stars akiwa na magoli 25.
Mrisho Ngassa amefunga ndoa na mrembo Ladhia
Mngazija Tegeta mjini Dar es Salaam mwaka 2014. Hii ni ndoa ya pili kwa mchezaji
huyo wa Yanga SC, ambaye alioa baada ya kuachana na mkewe wa awali.
Ngassa
ndie mchezaji wa pekee kutoka Tanzania aliewahi kucheza dhidi ya Manchester
united wakati akifanya majaribio ndani ya klabu ya Setter sounders ya marekani.
Katika
mchezo huoNgassa aliingia uwanjani kipindi cha pili katika dakika ya 76
na nusura awafunge mabingwahao
katika dakika ya 89
baada ya kupiga
shuti kali lililogonga mwamba.
Katika mechi hiyo iliyochezwa kwenye uwanja wa CenturyLink jijini Washington, Manchester ilifunga bao moja katika kipindi cha kwanza na mabao sita yakifungwa katika kipindi cha pili.
Katika mabao hayo, matatu yakiwekwa kwenye kamba na Wayne Rooney aliyeingia kipindi cha pili huku Gabriel Obertan akikamilisha idadi ya mabao hayo dakika ya 89.
Kipindi cha pili kilikuwa cha kasi huku kikiwa na sura mpya ambapo Manchester Unitedwalimuingiza Rooney huku Seattle Sounders wakibadili kipa Kasey Keller na kumuingiza
Terry Boss.
Katika mechi hiyo iliyochezwa kwenye uwanja wa CenturyLink jijini Washington, Manchester ilifunga bao moja katika kipindi cha kwanza na mabao sita yakifungwa katika kipindi cha pili.
Katika mabao hayo, matatu yakiwekwa kwenye kamba na Wayne Rooney aliyeingia kipindi cha pili huku Gabriel Obertan akikamilisha idadi ya mabao hayo dakika ya 89.
Kipindi cha pili kilikuwa cha kasi huku kikiwa na sura mpya ambapo Manchester Unitedwalimuingiza Rooney huku Seattle Sounders wakibadili kipa Kasey Keller na kumuingiza
Terry Boss.
Ukiachana
na Obertan na Rooney aliyefunga 'hat trick' katika dakika za 52, 69 na 72,wachezaji
wengine waliofunga
ambao katika mchezo huo ni Michael Owen (dk. 15), Mame Biram Diouf (dk. 49) na
Ji-Sung Park (dk. 71).
No comments:
Post a Comment