Mwanamama Jonesia Rukya, mhaya mpaka kwa wazungu. - ALEX MWENDATZ

Breaking

Sunday, January 6, 2019

Mwanamama Jonesia Rukya, mhaya mpaka kwa wazungu.




Na Alex Mwenda
Kuna waamuzi wengi ambao wamefanikiwa katika maisha ya uchezeshaji wa mpira wa miguu na kufanikiwa kutengenezaa majina katika ulimwengu huu wa soka na kujitengenezea umaarufu mkubwa pamoja na kuingiza pesa nyingi sana.

Hii leo ukizungumzia waamuzi maarufu duniani utasema Michael Oliver, Antony Tyler na waamuzi wengine wengi zaidi.
Hapa nchini Tanzania waamuzi waliopata umaarufu ni wengi akiwemo Israel Mujuni Nkongo, Joseph Mapunda, Herry Sasi, Hans mabena na wengine wengi.

Kazi ya uamuzi ni yenye lawama na ubabaishi mtupu kwa wale wasiojua kutafsiri sheria kumi na saba za mchezo wa soka, mwamuzi Jonas Eriksson kutoka sweeden ndie mwamuzi milionea zaidi duniani, na kuna wengine wameshindwa kutafsiri sheria 17za mchezo wa soka na kushuhswa hadhi zao.

Keysports ndani ya shujaawetu tuna mwangazia mwaamuzi wa kike alieleta mapinduzi makubwa katika ngazi hii ya uamuzi wa mpira wa miguu nchini, Jonesia Rukya.
Jina lake halisi ni Jonesia Rukya Kabakama alizaliwa mkoani Kagera Kaskazini magharibi mwa Tanzania, ambapo alisoma na kumaliza elimu yake ya msingi na sekondari mkoani humo.

Mwaka 2006 Jonesia Rukya alianza rasmi kujihusisha na masuala ya mchezo wa soka akiwa kama mchezaji katika timu ya hukohuko mkoani Kagera.

Baada ya kuona hakuna mafanikio yoyote aliamua kuacha na kuanza kujifunza masuala ya uamuzi jamba ambalo lilimtenganisha na sehemu kubwa ya familiaa yake kutokana na familia yake kutopenda anachokifanya.
Hakukata tamaa na mtu pekee aliekuwa akimsaidia na kumsapoti ni bibi yake jambo ambalo liliendelea kumtia nguvu kutokana na mchezo huu kuwa ndani ya damu yake.

Tangu mwaka 2006 alichezesha mechi za madaraja ya chini mpaka mwaka 2011 ambapo aliinuliwa na kupandishwa kuchezesha ligi daraja la kwanza mechi kati ya Rhino rangers vs AFC mchezo uliopigwa mkoani Arusha.
Rasmi mwaka 2014 alichaguliwa kuchezesha mechi ya Mtani jembe kati ya Yanga vs Simba, kitu ambacho kilimpa umaarufu na kujiamini zaidi na hapo ndipo fursa zingine zilifunguliwa kwa mwanamama huyu mashughuri zaidi barani Afrika na ulimwenguni kwote.

Alisimama pia katika derby ya Simba na Yanga September 30 mwaka jana katika mchezo ulipigwa uwanja wa taifa na kumalizika kwa sare ya bila kufungana.
Jonesia Rukya kabla ya kuwa mwamuzi nchini Tanzania, alikuwa mwalimu na mjasiliamali na aliweza kumudu vitu vyote viwili kwa wakati mmoja japo ilikuwa ni changamoto kubwa kwake.

Jonesia amepata nafasi ya kuchezesha michuano mikubwa AFrika ya kinamama, mwaka 2017 alichezesha michuano ya AFCON ya kina mama nchoni Cameroon, na mwaka 2018 alikuwepo pia nchini Ghana katika michuano hiyo.

Alichezesha michezo miwili, Mali na Cameroon hatua na makundi pamoja na Afrika kusini na Mali hatua ya nusu fainali.
Jonesia Rukya pia ni miongoni mwa waamuzi wachache watakaochezesha michuano ya kombe la dunia kwa wanawake mwaka huu nchini Ureno.

………. Kutoka kwa wahaya mpaka kwa wazungu, Huyu ndie shujaa wetu kwa siku ya leo anaitwa Jonesia Rukya Kabakama mwamuzi wa mchezo wa soka hapa 

No comments:

Post a Comment