S
![Image result for MTIBWA SUGAR](https://i0.wp.com/soka360.co.tz/wp-content/uploads/2016/04/Yanga_Mtibwa_02.jpg)
Ofisa Habari wa Mtibwa Sugar, Thobias Kifaru alisema kuwa adhabu yao hiyo ilishaisha siku nyingi na amewataka wale wote wanaowapotosha mashabiki wao kuacha mara moja kufanya hivyo. “Adhabu hiyo ilishaisha siku nyingi, kwani tulifungiwa miaka mitatu kutoshiriki michuano ya CAF,
kutokana na kosa hilo la kutoenda Afrika Kusini kucheza na Santos, kwa hiyo wanasema bado tumefungiwa tunaomba waache mara moja kuwadanganya mashabiki wetu. “Tangu kipindi hicho mpaka sasa ni karibia miaka 15 kwa hiyo ni wazi kuwa adhabu yetu ilishaisha na sasa tunajiandaa kuhakikisha mwaka huu tunakuwa mabingwa wa Kombe la FA ili tuweze kuiwakilisha Tanzania katika michuano Kombe la Shirikisho Afrika kwa mara ya nne,” alisema Kifaru. Mara ya kwanza kwa Mtibwa Sugar kushiriki michuano hiyo ilikuwa mwaka, 2001, kisha ikashiriki 2002 na mara ya mwisho ilikuwa ni 2003, katika miaka hiyo yote ilikuwa ikishia hatua ya pili ya michuano hiyo.
No comments:
Post a Comment