MAJIMAJI YAFUFUA MATUMAINI YA KUSALIA LIGI KUU MSIMU UJAO - ALEX MWENDATZ

Breaking

Wednesday, April 11, 2018

MAJIMAJI YAFUFUA MATUMAINI YA KUSALIA LIGI KUU MSIMU UJAO


Na Alex Mwenda-Songea
Majimaji hii leo wameweza kushinda ugenini dhidi ya Stend united kwa mabao 3-1.
 Image result for MAJIMAJI
Mabao ya Lucas kikoti, Peter Mapunda na Jerson Tegete likiwa ni bao lake la pili la msimu huu wa VPL, lakini ni bao lake la tatu tangu asajiliwe na Majimaji.
Mara ya mwisho majimaji kupata ushindi alipata dhidi ya Stend united uwanja wa majimaji mjini songea 2-1.

Tegete anakuwa sawa kwa magoli na ndugu yake Ngassa ambaye pia na mabao mawili, juzi tuu kafunga pia leo Tegette kafunga. Peter Mapunda ni goli lake la 4 msimu huu, kinara ni Marcelo Kaheza Boniventure mwenye goli 9.

Kwa matokeo haya Majimaji wanapanda kwa nafasi moja hadi nafasi ya 15 kwa alama 19, nyuma ya Njombe Mji wenye alama 18 baada ya hii leo kupoteza mbele ya Mbao fc.

Majimaji watashuka tena dimbani tarehe 15 mwezi huu kuwavaa Mbao fc katika uwanja wa Ccm Kirumba mkoani Mwanza, kasha kuwasubili Ruvu shooting tarehe 28 mwezi huu, na tarehe 5 mwezi wa 5 watawakaribisha Mtibwa.


No comments:

Post a Comment