Wakali wa muziki wa Bongo Fleva nchini, Rich Mavoko & Nay wa Mitego wamejikuta
wakijibizana mitandaoni baada ya Mavoko kutupia picha na maneno
yaliashiria ujio wa ngoma yake mpya wakati akisikilizia hali ya kisiasa
hapa nchini kwa sasa.
Hitmaker huyo ameonjesha picha ya kile kinachoonekana kuwa ni video yake mpya na kuandika: “Haya Mkimaliza Mambo Zenu Za Siasa Mtupe Tarehe Na Sisi Tufumue Hiii #Showme”
Baada ya Post hiyo Saa 18 baadaye, Nay wa
Mitego naye akachukua picha ile ile aliyotupia Mavoko, aka-repost na
kuandika huku akitamba kuwa ngoma pekee inayoweza kutusua kwa sasa ni
ngoma yake ya Wapo. “NAOMBA MUENDELEE KUSUBILI, MAY BE MPAKA MWAKANI 2018, NDO MTAANZA KUJISHUGHULISHA NA MASWALA YA KUWAIMBIA WANA NCHI”.
Baada ya kutoa maneno hayo, Nay alitumia fursa hiyo kwa kumuonya Diamond Platnumz kwa kumtumia salamu zilizosomeka hivi.. “MWAMBIENI
NA BABA YENU PIA AWE MPOLE KWA SASA ALEE WATOTO. KAZI TULIYO NAYO
IKIENDA SAWA TUTA WARUHUSU MUENDELEE KUBURUDISHA WANA NCHI. TUNATAKA
MAMBO YAENDA SAWA KWANZA”.
No comments:
Post a Comment