NI UFARANSA AU UBELGIJI NUSU FAINALI YA KOMBE LA DUNIA? HAWA NI MARAFIKI TANGU UDOGONI - ALEX MWENDATZ

Breaking

Monday, July 9, 2018

NI UFARANSA AU UBELGIJI NUSU FAINALI YA KOMBE LA DUNIA? HAWA NI MARAFIKI TANGU UDOGONI

Na Alex Mwenda-Songea
Image result for belgium vs france PREVIOUS RESULTS

Michuano ya kombe la dunia ilianza kutimua vumbi mnamo miaka ya 1930 huko nchini Uruguay na kuwashuhudia wenyeji wakilitwaa kombe hilo lakini wakarudia tena 1950 kwa kulitwaa tena na ndo ilikuwa mara yao ya mwisho kuweka makwapani taji hilo kubwa katika mchezo wa soka.

Mwaka 2018 Russia ndio wameandaa kombe la dunia na kushudia mengi ya kitokea kuondolewa kwa Messi na Argentina yake kadharika Ronaldo na Ureno yake bila kusahau Neymar na Brazil yake.

Keysports inawakumbusha kuwa hizo habari za kutolewa kwa mastaa wakubwa hazina utamu sana kama kuelekea mechi ya nusu fainali ya kwanza kati ya Ufaransa na Ubelgiji unajua nani atasonga au nani atamtambia mwenzake??
Picha ya hawa watu ilianza mnamo mwaka 1904 ambapo timu hizi zilitoka sare ya mabao 3-3 pale nchini Ubelgiji ilikuwa ni siku ya wafanyakazi namaanisha tarehe 1.5.1904

Hizi timu hazina uhasama bali ni marafiki wakubwa sana tangu urafiki wao ulipoanza mnamo mwaka 1904. Baada ya ile namjua namjua na matokeo kwenda sare wakaomba tena mechi ya kirafiki ili urafiki wao uzidi kudumu mwaka huo huo Ufaransa walinogewa na mchezo mtamu wa wapinzani wao Ubelgiji kutokana na utamu wa mabao 3-3.

Ubelgiji walikubali ombi lao na kurudia mechi, sio kwa Afrika tuu tamaduni hii ya kunogewa na mchezo na matokeo kumbe ilikuwepo pia miaka hiyo. Nakumbuka pia timu za magagura, lusonga na hata litisha na magima minogo ilikuwa sana wakati ambao Alex Mwenda Daady anatamba kwelikweli na yimu mbalimbali ikiwepo Masangu fc ya huko Magagura.

Tarehe 7.5.1904 walishuka dimbani tena na Ubelgiji kushinda mabao 7-0 hapo ndio Ufaransa walipoamka kisoka na kuamini kumbe watakiwa kuwa serious uwanjani, walirejea makwao kwa hudhuni kubwa sana na kaahidi kuwa undugu wao utaendelea na mwaka 1906 Ufaransa waliwaarika ubelgiji na wakiwa nyumbani waliduwazwa kwa bao 5-0.
Image result for belgium vs france PREVIOUS RESULTS
Hapo ndipo Ufaransa waliona kuwa hapana undugu ndani ya dakika 90 watu wapo makini sana mwaka 1907 Ufaransa walishuka tena dimbani dhidi ya ubelgiji nchini ubelgiji na Ufaransa kushinda kwa magoli 2-1..Unaweza kusema kuwa Ubelgiji waliamua kuwaachia tuu Ufaransa maana mpaka dakika za mwishoni mwa mchezo walikuwa nyuma kwa goli 1-0.
Hizi timu mbili zimekutana mara 73 tangu mwaka 1904, na Ubelgiji wao wakishinda mara 30 kwenda sare mara 19, huku Ufaransa wao wakishinda mara 24.

Kwa mara zote Ubelgiji ndie anaeshikiria rekodi ya kumfunga Ufaransa magoli mengi zaidi  mwaka 1905 ushindi wa mabao 7-0 lakini wakairudia tena rekodi hiyo mwaka 1911 wakishinda ubelgiji kwa goli 7-1.
Ubelgiji waliifunga pia Ufaransa magoli 6-1, na Ufaransa wao wameshikiria rekodi ya kuifunga ubelgiji mabao 5-3 mwaka 1938.
Rekodi zinaonesha katika michuano ya kombe la dunia timu hizi zimekutana mara 5 na Ufaransa wakishinda mara 3, sare mara moja na ubelgiji wakishinda mara 1 pekee.
Image result for belgium vs france PREVIOUS RESULTS
Taswira hii inaonesha kuwa Ufaransa nafasi ya kutinga fainali ni kubwa kuliko Ubelgiji japo wataalamu wa masuala ya utabiri nao wakiipa Ufaransa nafasi ya kushinda kwa 39% droo 30% na ubelgiji 31%

Mara ya mwisho timu hizi kukutana ilikuwa ni mwaka 2015 tarehe 7/6 ambapo Ubelgiji waliitambia Ufaransa kwa magoli 4-3.
Berther Conte ni shabiki mkubwa sana wa Killian mbape Rotin hana utofauti na Salama Idd Maridadi lakini nawaambia nusu fainali hii tuheshimiane kwanza.
Huku Lukaku, hapa Griezman, pale Hazard kule Mbape Lotini, hatoki mtuuuu hapa Rloris hapa Courtious.

Makala hii imeandaliwa na Alex Mwenda ambaye ni mtangazaji wa kipindi cha michezo kutoka KEYFM SONGEA pia mtangazaji wa mpira wa miguu.


No comments:

Post a Comment