
Ofisa wa Habari wa TFF, Clifford Mario Ndimbo, amekanusha taarifa hizo huku akisema Yanga wamemtumia kiongozi huyo wa matawi kuzungumza wakati hakuwa na mamlaka ya kufanya hivyo.
Ndimbo amesema kuwa Yanga wanajua kila kitu kuhusiana na deni hilo na hawakuwa na sababu ya kumtumia mtu ambaye hafahamu chochote kuhusiana na suala hilo hivyo watapaswa kutoa majibu ya kwanini wamemtumia.
Mbali na hilo, Ndimbo amesema pia kuwa ni kweli walizuia fedha zao za mapato zilizopatikana katika mchezo wa Simba na Yanga kutokana na deni ambalo wao wanadaiwa hivyo ikabidi wawakate.
Mwisho Ndimbo ameeleza kuwa TFF inaidai Yanga hivyo huku akieleza imesitikishwa na malalamiko ya mtu ambaye hakuwa na mamlaka ya kulisemea suala hilo wakati Yanga wanajua kila kitu.
No comments:
Post a Comment