Gold Goast 2018: Wanariadha wa Afrika Mashariki kupambana Jumatatu mbio za mita 10,000 - ALEX MWENDATZ

Breaking

Sunday, April 8, 2018

Gold Goast 2018: Wanariadha wa Afrika Mashariki kupambana Jumatatu mbio za mita 10,000


Sandrafelis Chebet
Image captionSandrafelis Chebet mkimbiaji kutoka Kenya anategemewa sana kufanya vema kwenye mbio za mita 10, 000 wanawake Gold Coast
Wanariadha wa Kenya, Tanzania, Rwanda na Uganda wanatarajiwa kupambana vikali Jumatatu wiki hii katika fainali ya mbio za mita elfu kumi kwenye michezo ya Jumuiya ya Madolamjini Gold Goast.
Kuna kivumbi hapo kwani Wakenya wana hasira mno ya kulipiza kisasi kutokana na ushindi wa Joshua Cheptegei wa Uganda Jumapili mbio za mita elfu tano.
Kuna kivumbi hapo kwani Wakenya wana hasira mno ya kulipiza kisasi kutokana na ushindi wa Joshua Cheptegei wa Uganda Jumapili mbio za mita elfu tano.
Mkimbiaji wa Rwanda Salome Nyirarukundo
Image captionMkimbiaji wa Rwanda Salome Nyirarukundo anatarajiwa kuwapa kibarua kikali wapinzani wake baada ya kufanya mazoezi na wakimbiaji wa Kenya eneo la bunde la ufa.
Ni ushindi ambao haujawafurahisha hasa kuangushwa na mkimbiaji wa Uganda ambao kwa miaka mingi wamekua hawababaishi wakimbiaji wa Kenya.
Wakimbiaji wa Kenya wanaotegemewa sana kufanya vyema ni Sandrafelis Chebet ambaye alizaliwa Kericho Januari tarehe 20 1998 ,Stacy Ndiwa na Beatrice Mutai..
Failuna Matanga mkimbiaji kutoka Tanzania
Image captionFailuna Matanga mkimbiaji kutoka Tanzania pia atashiriki mbio za mita 10,000
Mashabiki katika michezo ya Jumiya ya Madola 2018 Gold Coast
Image captionUwanja uliosheheni mashabiki wa michezo ya Jumuiya ya Madola mwaka 2018 -Gold Goast
Wanakabiliwa na upinzani mkali kutoka kwa mkimbiaji wa Rwanda Salome Nyirarukundo ambaye amefanya mazoezi nao eneo la bunde la ufa..
Kutoka Tanzania kuna Failuna Matanga na waakilishi wa Uganda Mercyline Chelangat, Juliet Chekwel na Stella Chesang.

No comments:

Post a Comment