Nahodha wa Liverpool Jordan Henderson amegoma kuwalinganisha MO Salah na shujaa wa zamani wa Anfield Luis Suarez.
" Wote ni wachezaji wazuri sana kwa haki zao stahiki na huwezi kuwalinganisha."
" Ni wachezaji tofauti. Najua kwamba wote wanafunga sana magoli na wanajituma sana pindi wakiwa hawana mpira lakini ni ngumu kuwalinganisha ."
" Luis alihamia Barcelona na anafanya vizuri sana . Ni mchezaji wa daraja la juu sana na najisikia fahari kuwahi kucheza nae."
" Lakini MO msimu huu amekuwa wa ajabu sana. Wa ajabu kweli kweli . Anafanya kila wiki bila kushindwa."
No comments:
Post a Comment