Na Alex Mwenda
Leo shujaa wetu tunamwangazia
staa wa kimataifa wa Ufaransa aliepata kuwika sana katika historia ya soka
duniani, ladies and gentlemen tunamleta kwenu Thierry
Henry……
Thierry Daniel Henry alizaliwa tarehe 17.8.1977
Ni mchezaji mstaafu wa timu ya taifa ya
Ufaransa aliepata kucheza kama mchambulaji na hivi sasa ni kovha msaisizi wa
taifa la Ubelgiji.
Amepata kucheza katika vilabu vikuba kama
Monaco, Juventus, Barcelona, New York Red Bulls, na alitumia miaka 8 katika
klabu ya Arsenal ambae ni mfungaji wa muda wote katika klabu hiyo ya washika
bunduki.
Henry alianza maisha yake ya maisha ya
soka la kulipwa katika klabu ya Monaco 1994 kiwango kizuri kilimfanya aitwe
katika kikosi cha timu ya taifa ya Ufaransa 1998, baada ya hapo alisain I
mkataba kuitumikia Juventus baada ya mwaka mmoja alijiunga na ligi kuu nchini
England katika klabu ya Arsenal chini ya kocha Arsene Wenger na kutengeneza
jina kubwa na kuwa world class player na kuwa mfungaji bora wa muda wote
Arsenal akifunga magoli 228 katika mashindano yote.
Alipata kushinda mataji mawili ya ligi kuu
england na mataji matatu ya FA kwa vilabu kwa miaka ya 2003 na 2004. Herny
alichaguliwa kuwa mchezaji bora wa FIFA world player of the year, na
aliorodheshwa katika tuzo za mchezaji bora wa kigeni England PFA Players' Player of
the Year , FWA Footballer of the
Year
Katika
mwezi june 2017 baada ya kudumu kwa washika bunduki wa Arsenal alihamia kwa
miamba wa Barcelona kwa ada ya uhamisho wa uro 24 milioni. Mwaka 2009 aliweka
rekodi ya kutwaa La Liga, Copa del Rey na UEFA Champions League.
Aidha
alipata mafanikio mengine baada ya kushinda Supercopa de España,
UEFA Super Cup na FIFA Club World Cup.
Kwa
ujumla Henry aliorodheshwa katika kikosi bora cha Uefa kwa miaka mitano
mfururizo. Mwaka 2010 alijiunga na klabu ya New York Red
Bulls ambayo inashiriki ligi kuu ya Marekani Major League Soccer, na aliweza kushinda ubingwa wa Eastern Conference
na kuwa mchezaji bora katika mwaka huo
wa 2010.
Mwaka
2012-2013 alirejea tena Arsenal kwa mkopo wa miezi miwili na baada ya hapo
alirejea tena Marekani katika klabu yake ya New York Red Bulls na alishinda MLS Supporters' Shield.
Henry
alifurahia mafanikio ya timu ya taifa ya Ufaransa baada ya kushinda kombe la
dunia 1998, uefa euro 2000, na kombe la mabara 2003. Mwaka 2007 aliwashangaza
wengi baada ya kuvunja rekodi ya aliekuwa staa wa timu hiyo Michelle Platin kwa
kuwa mfungaji bora wa muda wote wa timu ya taifa baada ya kucheza michezo 123
na kufunga magoli 51.
Henry
alistaafu rasmi baada ya mashindano ya kombe la dunia mwaka 2010 Afrika ya
kusini. Henry alikuwa moja kati ya wachezaji ambao walifanya biashara kubwa
sana kupitia soka na aliorodheshwa kuwa wa tisa mnamo mwaka 2006.
Mwaka
2016 mwezi wa nane aliteuliwa kuwa kocha msaidizi wa timu ya taifa ya Ubelgiji
kusaidia na kocha mkuu Roberto MartÃnez pamoja na Graeme Jones.
Henry
anatoka katika koo ya Antillean na baba yake ni Antoine, ambae anatokea katika kisiwa cha Guadeloupe na mama yake ni Maryse, amabye ni mwenyeji wa Martinique
Alizaliwa
na kukulia katika mji wa Les Ulis amabao unapatikana katika mji wa Paris , Alipokuwa na
miaka 7 Henry alionesha kiwango cha
kuvutia sana kilichomfanya wakala Claude Chezelle kumjumuisha katika timu ya
mtaani ya CO Les Ulis.
Baba
yake alimsisitiza sana kufanya mazoezi kwa bidii tangu akiwa bado mdogo, na
alijiunga katika klabu ya US Palaiseau katika mwaka 1989, baada ya mwaka baba
yake alifungashiwa virago na Henry aliondoka na kujiunga na ES Viry-Châtillon na kucheza kwa miaka miwili mpaka alipopata kuonekana na kujiunga na US Palaiseau ambapo kocha wa timu hiyo Jean-Marie Panza kum[a nafasi zaidi, hapo
ndoto zake zilianza kutimia.
Ametunukiwa
tuzo mbalimbali wakati akiwa na vilabu tofauti
Monaco
Arsenal
Barcelona
New York Red Bulls
·
Katika timu ya taifa
Henry ameshinda
Tuzo
binafsi
·
·
·
Hizo ni baadhi ya tuzo
amechukua zaidi ya tuzo 55.
No comments:
Post a Comment