GARETH SOUTHGATE NAWAJUA WACHEZAJI 19-20 WA KOMBE LA DUNIA KATIKA KIKOSI CHA TIMU YA TAIFA YA UINGEREZA - ALEX MWENDATZ

Breaking

Wednesday, March 28, 2018

GARETH SOUTHGATE NAWAJUA WACHEZAJI 19-20 WA KOMBE LA DUNIA KATIKA KIKOSI CHA TIMU YA TAIFA YA UINGEREZA

Image result for GARETH SOUTHGATE
Kocha wa Timu ya taifa ya Uingereza, Gareth Southgate amesisitiza kwamba anajua majina 19 au 20 ya wachezaji ambao watapanda ndege kwenda Urusi baada ya kushuhudia kikosi chake kikipata sare ya 1-1 dhidi ya Italia jana usiku.

Mechi ya jana ilikuwa ya mwisho kwa wachezaji wa Uingereza kupata nafasi zao za kwenda Urusi , ambapo kikosi cha awali cha wachezaji 35 kitawasilishwa FIFA Mei 14, na kikosi cha mwisho cha wachezaji 23 wanaotakiwa kinatakiwa kiwasilishwe Juni 4.

" Kumekuwa na kiwango kizuri sana kwa baadhi ya wachezaji ambao wamepata nafasi zao kwenye kikosi , 19 au 20 kati yao imekuwa wazi , lakini mara nyingi imekuwa ni wakina nani wanaofuata kama tukipata tatizo katika eneo fulani."

" Vitu tulivyojaribu tumejifunza sana , kitu ambacho kimenivutia sana ni kwamba vijana wamekuwa wakitatua matatizo wenyewe ndani ya uwanja "

" Najisikia fahari sana kuongoza kundi hili la wachezaji katika mashindano ya kombe la Dunia." 

No comments:

Post a Comment