AZAM YATANGAZA KUACHANA NA MUDATHIR YAHAYA - ALEX MWENDATZ

Breaking

Wednesday, March 28, 2018

AZAM YATANGAZA KUACHANA NA MUDATHIR YAHAYA


Uongozi wa klabu ya Azam FC umetangaza kuwa mchezaji wake, Mudathir Yahaya, yupo huru kuelekea sehemu nyingine baada ya kumaliza mkataba wake.

Kupitia Afisa Habari wa Azam FC, Jaffer Idd, amesema mchezaji huyo yupo huru hivi sasa na kama timu nyingine ikimuhitaji, ruksa kumsajili.

Yahaya aliondoka Azam FC na kutimkia Singida United kwa mkopo Julai 17 2017 baada ya mkataba wake wa miezi mitatu uliokuwa umesalia ndani ya Azam kumalizika.

Mpaka sasa Yahaya yuko Singida United akijiandaa na wenzake kuelekea mchezo wa Kombe la Shirikisho utakaopigwa Aprili Mosi 2018 dhidi ya Yanga kwenye Uwanja wa Namfua.

No comments:

Post a Comment