Arsene Wenger wazungu wanamuita “White Mugabe” wakimaanisha
ni mzungu mwenye tabia za Robert Mugabe. Ni miaka 88 sasa imepita tangu
Arsenal wafungwe magoli matatu tatu katika michezo minne mfululizo ya
ugenini na mechi dhidi ya Palace Wenger amevunja rekodi hiyo, kwa
takwimu zifuatazo zinaonesha ni lazima Arsenal walistahili kipigo kutoka
kwa Palace.
1.Arsenal hawakupiga hata shuti moja golini kwa Crystal Palace
kipindi cha pili. Huwezi kupata ushindi huku washambuliaji wako
hawaoneshi utashindaje, timu nzima ya Arsenal wakiongozwa na
mshambuliaji wao Alexis Sanchez hawakupiga hata shuti moja golini mwa
Crystal Palace katika kupindi cha pili.
2.Shkordan Mustafi hakufanikiwa tackle hata moja katika 6 alizofanya.
Kwa vijana wa huku tunaita “katoa boko”, kwani Mustafi alikuwa
akipambana kufanya ukabaji lakini takwimu zinaonesha katika tackle zake 6
alizojaribu kufanya, alizipoteza zote.
3.Mamadou Sakho ametengeneza nafasi nyingi kuliko Ozil na Sanchez.
Katika mchezo huo Mesut Ozil hakutengeneza hata nafasi moja huku Sanchez
akitengeneza moja, wakati beki wa Crystal Palace Mamadou Sakho
alitengeneza nafasi mbili.
4.Arsenal wameruhusu magoli matatu kwa kila mchezo wa ugenini katika
mechi 3 kabla ya kukutana na Crystal Palace. Walifungwa 3 na West Brom
ugenini, wakafungwa 3 na Liverpool ugenini, wakafungwa 3 na Chelsea
ugenini hii iliwapa imani Palace nao kuwafunga 3, hii ikiwa rekodi mbaya
kwao tangu mwaka 1929.
5.Arsenal wamefungwa magoli mengi kuliko timu iliyoko nafasi ya 19.
Arsenal walioko nafasi ya 6 hadi sasa wamefungwa magoli 39 huku
Middlesbrough walioko nafasi ya 19 katika msimamo wa ligi hadi sasa
wamefungwa mabao 37.
Tuesday, April 11, 2017
New
Kwa takwimu hizi Arsenal walistahili kipigo kutoka kwa Palace
About SPORTS ROOM
SoraTemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of SoraTemplates is to provide the best quality blogger templates.
MICHEZO
Labels:
MICHEZO
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment