Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) inatarajiwa kuendelea
Alhamisi Aprili 13, 2017 kwa timu ya Mbeya City kuikaribisha African
Lyon ya Dar es Salaam kwenye Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.
Jumamosi ya Aprili 15, mwaka huu kutakuwa na michezo minne ambako
Stand United itakuwa mwenyeji wa Mtibwa Sugar ya Morogoro kwenye Uwanja
wa Kambarage mkoani Shinyanga wakati Toto Africans ya Mwanza itaialika
Simba SC ya Dar es Salaam kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.
Kadhalika siku hiyo ya Jumamosi, Majimaji ya Songea itakuwa mgeni wa Ruvu Shooting ya
Pwani kwenye Uwanja wa Mabatini mkoani Pwani ilihali JKT Ruvu ikiwa
kwenye Uwanja wake mpya wa nyumbani – Mkwakwani jijini Tanga itaialika
Azam ya Dar es Salaam.
Jumapili Aprili 6, mwaka huu Mbao itacheza na Tanzania Prisons kwenye
Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza huku Mwadui ikiwa mwenyeji wa
Ndanda FC ya Mtwara kwenye Uwanja wa Mwadui mkoani Shinyanga.
Tuesday, April 11, 2017
New
FAHAMU RATIBA YA LIGI KUU WEEKEND HIII
About SPORTS ROOM
SoraTemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of SoraTemplates is to provide the best quality blogger templates.
MICHEZO
Labels:
MICHEZO
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment