Watakaoweka rekodi Simba na Yanga - ALEX MWENDATZ

Breaking

Monday, February 20, 2017

Watakaoweka rekodi Simba na Yanga

Wakati timu mbili kongwe nchini, Simba na Yanga zinatarajiwa kupambana Jumamosi kwenye Uwanja wa Taifa kwenye mechi ya  mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Itakuwa ni mara ya pili kukutana mwaka huu, kwani zilipambana  kwenye hatua ya nusu fainali ya Kombe la Mapinduzi mjini Zanzibar  Januari.

Pia itakuwa ni mechi ya pili kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara, kwani zilikutana Oktoba Mosi mwaka jana kwenye mechi ya mzunguko  wa kwanza na kutoka sare ya bao 1-1.
Ni mechi itakayowafanya baadhi ya wachezaji waingie kwenye  rekodi mbali mbali za pambano la watani wa jadi.
Wafuatao ni wachezaji ambao kama wakicheza au kufunga  wataweka rekodi zao binafsi kwenye mechi hiyo.

 Daniel Agyei-Simba

Daniel AgyeiImage result for DANIEL AGREY WA SIMBA

Hapana shaka kuwa ndiye atakayekaa golini Februari 25. Ataweka  rekodi  ya kudaka mechi ya kwanza ya watani wa jadi kwenye mechi  za Ligi Kuu.
Pia itakuwa ni mara ya pili kukaa golini dhidi ya Yanga, kwani ameshafanya hivyo mjini Zanzibar, Kombe la Mapinduzi.

 Justine Zullu-Yanga

Justine Zullu ( Picha hisani )

Kama atacheza, itakuwa ni mechi ya kwanza ya watani wa jadi. Mchezaji huyo raia wa Zambia, alisajiliwa kipindi cha dirisha dogo katikati ya msimu huu.
 Ibrahim Ajibu-Simba

Ibrahim Hajib

Akifunga goli, litakuwa ni bao lake kwa kwanza kwenye mechi ya  Simba na Yanga. Hajawahi kufunga goli kwenye mechi ya watani wa jadi, tangu  aanze kuichezea Simba msimu wa 2014/15.
Obrey Chirwa-Yanga



Itakuwa ni mechi yake ya kwanza kuichezea Yanga dhidi ya Simba. Hakucheza kwenye mechi ya mzunguko wa kwanza. Akifunga bao  litakuwa la kwanza kuifunga Simba.
Shiza Kichuya-Simba



Akifunga goli, litakuwa la pili kuifunga Yanga kwenye mechi mbili  mfululizo. Ikumbukwe kuwa ndiye aliyefunga bao la kusawazisha kwenye  mechi ya mzunguko wa kwanza msimu huu, Oktoba Mosi, dakika ya  87.
Pia itakuwa ni mechi ya pili kuichezea Simba dhidi ya Yanga.
Donald Ngoma-Yanga



Straika huyu wa Yanga, kama akifunga goli litakuwa ni la pili kuifunga timu hiyo, tangu alipojiunga na timu hiyo msimu wa  2015/16.
Ngoma aliifungia Yanga goli dhidi ya Simba Februari 20, 2016, alipoukuta mpira uliorudishwa kizembe na Hassan Kessy, Yanga ikishinda mabao 2-0.
Laudit Mavugo-Simba



Atakuwa akicheza mechi yake ya pili dhidi ya Yanga kwenye mechi  za Ligi Kuu. Raia huyu wa Burundi, alicheza kwenye mechi ya mzunguko wa  kwanza, lakini alidhibitiwa vema na mabeki wa Yanga, na  hakung’ara kabisa.
Akifunga litakuwa ni goli lake la kwanza kwenye mechi za  mahasimu wa jadi.

Amissi Tambwe-Yanga

Akifanikiwa kufunga goli, litakuwa ni la nne mfululizo kuifunga  Simba kwenye mechi za Ligi Kuu Tanzania Bara.
Tambwe, aliyejiunga na Yanga akitokea Simba katikati ya msimu  wa 2014/15, amefunga goli moja kwenye mechi tatu mfululizo za ligi ambazo timu yake ilicheza dhidi ya Simba.
Bao lake la kwanza lilikuwa ni Septemba 26, 2015, Simba ikilala  kwa mabao 2-0 na mechi ya mzunguko wa pili Februari 20, 2016  akifunga, Yanga ikishinda tena mabao 2-0. Mechi zote ni za msimu  wa 2015/16.
Oktoba Mosi, 2016, mechi ya mzunguko wa kwanza msimu huu,  alifunga goli timu yake ikilazimishwa sare ya bao 1-1 dhidi ya  Simba.

Juma Luzio-Simba
Akifunga goli litakuwa ni la kwanza kwenye mechi ya watani wa  jadi. Straika huyo wa Kibongo, zamani akiichezea Mtibwa Sugar, ndiyo  kwanza amejiunga kwenye kipindi cha dirisha dogo msimu huu  akitokea Zesco ya Zambia kwa mkopo.

Simon Msuva-Yanga
Hajaifunga Simba goli lolote lile kwa misimu mitatu sasa. Mara ya mwisho kufunga bao dhidi ya Simba ilikuwa ni Aprili 19,  2014,
Ligi Kuu msimu wa 2013/14.
Amecheza mechi sita za watani wa jadi bila kufunga goli, licha ya kwamba ni mmoja wa wafungaji viongozi kwenye timu ya Yanga.
Akifunga goli Jumamosi, litakuwa ni goli lake la pili kuifunga Simba tangu alipojiunga na timu hiyo mwaka 2012 akitokea Moro United.

No comments:

Post a Comment