Singida United yapanda Ligi Kuu - ALEX MWENDATZ

Breaking

Saturday, February 11, 2017

Singida United yapanda Ligi Kuu

Klabu ya Singida United imepanda rasmi Ligi Kuu ya Vodacom msimu ujao,  baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2 – 0 dhidi ya waliokuwa wapinzani wao wa karibu Alliance Schools.
 Image result for SINGIDA UNITED
Singida United imefikisha pointi 30 ambazo haziwezi kufikiwa na timu yoyote kutoka kundi C, na kufanya msimu ujao wakazi wa mkoa huo kushuhudia uhondo wa VPL uwanja wa Namfua.

Katika mchezo mwingine Panone wametoka sare ya mabao 2 – 2 dhidi ya Rhino Rangers ya Tabora leo katika uwanja wa Ushirika mjini Moshi.

Kikosi cha Fred  Felix  Minziro kimefikisha pointi 30 huku wakiwa na mchezo mmoja mkononi, Alliance Schools 26, Rhino Rangers 25

Mpaka sasa timu mbili zimeshapanda kucheza Ligi Kuu msimu ujao, Lipuli kutoka kundi A na Singida United kutoka kundi C.

Timu moja inasuburiwa kutoka kundi B lenye upinzani kati ya Polisi Moro, Kinondoni Manispaa, Njombe Mji ikiwa imbakia michezo miwili kabla ya kumalizika kwa michezo ya kundi hilo.

No comments:

Post a Comment