Wawakilishi wa Rwanda katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika, APR
ya Rwanda wameweza kuwabana wapinzani wao, Zanaco FC ya Zambia na
kupata sare ya bila kufungana ugenini.
Katika pambano hilo lililopigwa leo, Zanaco walikaribia kupata bao la
kuongoza kupitia kwa Saith Sakala lakini mshambuliaji huyo alishindwa
kulenga lango na kupoteza nafasi dakika ya 39.
APR walijibu mapigo dakika tatu baadaye kupitia kwa Patrick Sibomana
kufuatia mpira wa kona lakini walinzi wa Zanaco walifanikiwa kuokoa
hatari hio.
Dakika moja kabla ya mapumziko, alikuwa ni Sibomana tena aliyekaribia
kupata bao pale shuti lake lililopotua katika nyavu ndogo kwa ahueni ya
wenyeji wao.
Kwa matokeo hayo, APR ambao walitolewa na Yanga mwaka jana katika
hatua ya raundi ya kwanza watahitaji ushindi wa aina yoyote kusonga
mbele.
Pambano la marudiano litachezwa Jumamosi ijayo jijini Kigali, Rwanda
katika uwanja wa Amahoro. Mshindi baina ya APR na Zanaco atakutana na
mshindi baina ya wawakilishi wa Tanzania, Yanga na wawakilishi wa Comoro
Ngaya ambao wanacheza mechi ya awali kesho.
Saturday, February 11, 2017
New
APR wajiweka sawa kurudiana na Yanga, waibana Zanaco
About SPORTS ROOM
SoraTemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of SoraTemplates is to provide the best quality blogger templates.
MICHEZO
Labels:
MICHEZO
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment