MWAMUZI ALIETANGAZA KUJIUZURU ABADILI GIA - ALEX MWENDATZ

Breaking

Tuesday, February 21, 2017

MWAMUZI ALIETANGAZA KUJIUZURU ABADILI GIA

Mwamuzi Mark Clattenburg ameamua kubadili uamuzi wake wa kuachana na Ligi Kuu Uingereza mara moja.

Awali Clattenburg alipanga kutochezesha mechi zaidi Ligi Kuu Uingereza kufuatia kuingia mkataba mnono wa kuwa mkuu wa kitengo cha waamuzi nchini Saudia Arabia.

 Image result
Baada ya masahauriano baina yake na viongozi wa kitengo cha waamuzi Uingereza, Clattenburg ataendelea kuchezesha mechi za Ligi Kuu hadi mwisho wa msimu huu.

Ataanza majukumu yake nchini Saudia Arabia baada ya kumalizika msimu. Tayari amerudi Uingereza na anatarajiwa kuchezesha pambano kati ya West Borom na Bournemouth siku ya Jumamosi.
Hata hivyo anaweza asipangwe kuchezesha mechi kubwa kama ile ya Arsena na Liverpool ambayo kwa kawaida huwa anapewa kuchezesha kutokana na ubora wake.

No comments:

Post a Comment