GODFREY BONY ATUTOKA - ALEX MWENDATZ

Breaking

Friday, February 17, 2017

GODFREY BONY ATUTOKA

Godfrey Bonny kiungo wa zamai wa klabu ya Yanga na timu ya taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ amefariki dunia alfajiri ya leo huko nyumbani kwao Mbeya.

February 2, 2017 mtandao huu uliandika habari ya kuumwa kwa Godfrey Bonny ambaye alikuwa amelazwa hospitali ya Rungwe-Tukuyu Mbeya alikokuwa akipatiwa matibabu.
 Image result for GODFREY BONY
Wakati akicheza soka, Bonny aliwahi kuvitumikia vilabu vya Tanzania Prisons na Yanga kwa vipindi tofauti pamoja na timu ya taifa ya taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’
.
SPORTS WEEKENDA inaungana na wadau wengine wa soka na michezo kwa ujumla, kutoa pole kwa familia ya Godfrey Bonny kwenye kipindi hiki kigumu cha msiba wa mpendwa wetu.
R.I.P Godfrey Bonny, hakika tutaendelea kukumbuka kile ulichokifanya katika soka la Tanzania.

No comments:

Post a Comment