Mchezaji wetu Daniel Lyanga hajatungiwa miezi sita kucheza soka,
Klabu yetu ya Singida United ilifuata taratibu zote za usajili wa mchezaji
Daniel Reuben Lyanga, usajili ulishirikisha pande zote mbili kati ya Fanja Fc
na Singida United ikiwemo kulipa fidia za gharama wa mkataba wake uliokuwa
umebakia kule Fanja Fc.
Taratibu ambazo zilipekea klabu yetu kupata release letter ya mchezaji na kuendelea na hatua za kiusajili.
Kilichopo ni kwamba ITC ya Daniel
Lyanga ilichelewa kuja kutokana na dirisha la usajili kufungwa, hivyo FIFA
walituandikia barua kwamba ITC yake itakamilika hadi hapo dirisha kubwa la
usajili litakapofunguliwa hapa Tanzania ( kunzia July/2018). Daniel Lyanga
hajafungiwa na hivi tunategemea kumtumia kwenye michuano ambayo klabu yetu
inakwenda kushiriki nje ya nchi.
Tunaomba vyombo vya habari
kutumia taarifa rasmi kutoka vyanzo rasmi kwa maslahi ya mpira wa miguu hapa
nchini.
Singida United milango yetu ipo wazi kutoa ushirikiano kwa jambo lolote ambalo chombo cha habari kinataka kujua, kufahamu au kushauri.
Singida United milango yetu ipo wazi kutoa ushirikiano kwa jambo lolote ambalo chombo cha habari kinataka kujua, kufahamu au kushauri.
No comments:
Post a Comment