MAJIMAJI WAONDOENI MAKOCHA TIMU IBAKI LIGI KUU MSIMU UJAO - ALEX MWENDATZ

Breaking

Tuesday, March 27, 2018

MAJIMAJI WAONDOENI MAKOCHA TIMU IBAKI LIGI KUU MSIMU UJAO

Image result for majimaji


 Na Alex Mwenda
Wazee wa zamani walituachia misemo mingi yenye maana kwa ajili ya kuiasa jamii ili iwe katika mwenendo ambao ni mzuri zaidi.
Lakini kizazi cha siku hizi  ni ngumu kuamini misemo ya wazee wa kale kama chelewa chelewa utamkuta mwana si wako tena, ngoja ngoja yaumiza matumbo, na hata ule wa mficha maradhi kifo kitamuumbua.

Bado mnaficha  maradhi yenu ndani ya klabu ya MAJIMAJI msubili kifo kije kuwaumbua na watu wapate nafasi ya kuzungumza, kwani asiye sikia la mkuu huvunjika guu.
Kila shabiki na mnazi wa wanalizombe ukimhoji majibu atakayokupa juu ya MAJIMAJI ni tayari hana matumaini ya kuiona timu hii kwa msimu ujao

Mnawaludisha vipi mashabiki wa aina hii ambao tayari kwao mioyo yao imekufa, na matumaini hawana tena juu ya klabu yao???
Mwarobaini mnao nyie viongozi lakini lazima mkubali kuwa makocha wa timu wameishiwa mbinu za kubuni, leo hi timu imecheza michezo 22 imekusanya alama 16 bado mnaendelea kuwakumbatia watu kama hawa mkiwa bado mna matumaini ya kuwa watawapa alama 15 katika michezo iliyosalia hakika hii ni ndoto ya Bunuwasi.
Kama timu imeshindwa kupata ushindi wowote nje ya uwanja wa Majimaji mnatarajia miujiza ipi timu ipate matokeo nje ya majimaji hivi sasa??

Wakati wote timu imekuwa ikicheza vizuri sana lakini tatizo lipo kwenye benchi la ufundi, viongozi hamuwaoni hao na bado mnawakumbatia tuu, kumbukeni kuwa Nungunungu hakumbatiwi, au mnapenda kuona timu ikishuka daraja???

Niwakumbushe msimu wa 2014\2015 Tz prisonsi ilikuwa dhohofu bini hari ikiwa chini ya kocha Jumanne chale waliketi chini bila aibu walimtimua kocha wao na kumpa mikoba Abduri Mingange, Prisons ikabaki ligi kuu, na msimu uliofuata walimtimua, lakini jee kama wangeendelea kuwa nae leo hii wangekuwepo wapi????

Msimu uliopita  Ndanda fc walikuwa katika hali mbaya sana hali iliyoperekea wachezaji kutoroka kambini lakini walikaa chini kwa kushirikiana na aliekuwa mkuu wa mkoa wa Mtwara bi Halima Dendego na kumtimua kocha wao na kumpa mikoba Abduri Mingange ambae aliinusuru timu kushuka daraja na baada ya mipango kukamilika walimtimua Mingange.

Lazima tuukubali ukweli kuwa timu hii ya Majimaji tangu ipande daraja msimu wa 2015/2016 haijawahi kuwa na kocha bora kama Karl Ongala moja kati ya wakufunzi waliojijengea heshima kubwa sana katika soka la Tanzania.
Mnashindwaje kutenga milioni kadhaa tena mpo na mtu wa michezo ambae anawasaidia mbunge Damas Ndumbaro ambae ni msikivu sana hasa katika yale yote yaliyo mema, leo hii bado mnaamini kuwa benchi lenu la ufundi litawakomboa nawaambieni msaahau msipofanya mabadiriko.

Ule msemo usemao mkaidi hafaidi hadi siku ya iddi ulikuwa na maana kubwa sana tunaamini kuna makanjanja katika timu ya Majimaji ambao wao utawaona katika zile siku za mafungu na migao ya mapato ya mlangoni hata malupulupu mengineyo, sasa mnashindwa kujiongeza, makanjanja wenzenu huwa wanapigania timu ziendelee kuwepo katika ligi ili matumbo yao yapate unafuu, lakini kwenu mnawaza kurubuni kwa muda mfupi.

Hakuna soka wala vilabu visivyo na makanjanja ndani yake hata Simba, Yanga, Lipuli fc, Ndanda, Mwadui wajanja wajanja wapo lakini wana wao wana muono wa mbele hasa katika kuipigania timu kwa namna yeyote ile.
Mnakumbuka Njombe mji baada ya kupanda ligi walikuwa chini ya Hassan Banyai wakamtimua baada ya kuona timu inapata matokeo mabaya walifanya maamuzi, na kuwaachia Mlage wa kabange na Ally Bushiri, kwenu mbona bado hamna maamuzi?

Tatizo la kufanya kazi kimazoea na kishikaji ndo ambako kunaaribu taratibu za timu, lazima mtambue kuwa heshima ya klabu ni matokeo leo hii mnajipa kazi kubwa sana kwenda kuheshimika kanda ya ziwa kutokana na matokeo yenu.
Tujitafakari huko tunakoelekea mnadhani ni sahihi au tupambane hapa tulipo, tuliwataka muitishe mkutano hamkufanya hivyo, ina maana hamkuheshimu mchango na mawazo yetu, sasa tunawataka mfanye mabadiriko katika benchi lenu la ufundi na msipofanya hivyo msitarajie miujiza yoyote ile.

Wanaruvuma tutawalamu sana katika hilo na hata ikitokea mmeishusha daraja timu msione haya kujivua madaraka kwani muungwana huchutama anapokosea.

Niwakumbushe mlibugi katika mkataba na TING, mkala mwereka kwenye mkataba feki na SOKABET yote athari zake mmeziona, sasa na katika hili mkibugi basi kwa herini, na mtambue mnakoenda ni kugumu zaidi kwani yahitaji wazalendo haswa kusukuma gurudumu hili...
Msipo yafanyia kazi haya tukutane ligi daraja la kwanza msimu ujao. Haya yote ni mema tuu kwa faida ya Wanaruvuma wote.


No comments:

Post a Comment