Miongoni mwa Timu ambazo zilitokea kuwa tishio hapa nchini miaka
ya 1980 hadi 2000 ukiachana na Simba na yanga kwa wapenda soka lazima
ataikumbuka Maji Maji ya Songea Maarufu kwa Jina la Wanalizombe.
Maji Maji ambayo
Ilizaliwa rasmi mwaka 1977 kwa muunganiko wa timu mbali mbali mjini Songea
chini ya Mwasisi wa timu hiyo Dk Roulence Gama ilianza kupata umaarufu mkubwa
mwaka 1980 mwaka ambao timu hiyo ilipata nafasi ya kushiriki kwa mara ya kwanza
ligi Daraja la kwanza hapa nchini.
Jelamba viwanja imefanya
Mazunguzo Maalum na aliyewai kuwa Meneja wa Maji Maji Aly Mbalika Kuanzia mwaka
1997 pia Meneja wa Sasa Godfrey Ambros Mvula ambao Baba zao walikuwa watu
muhimu sana ndani ya Maji Maji Miaka ya 1980, Kwanza mzee Mbalika anaanza
kueleza histori ya timu hiyo kuanzia mwaka 1980 hadi 2001;-
“Mzee Gama baada ya
kuwasili Mkoani Ruvuma alianzisha azimio la Mlale akiwa kama mkuu wa mkoa
likiwa na maana ya kilimo Pamoja na michezo lakini kwa upande wa michezo
hakuenda mbali sana hasa alilenga zaidi mchezo wa mpira wa miguu akaazisha timu
ya Maji Maji na kujenga uwanja Wa Maji Maji uwanja ambapo vyumba vyote vya
uwanja huo aliwapangisha wachezaji wa Maji Maji Na kuwanunulia fenicha.
“Timu hiyo kwa mara ya
kwanza ilikuwa chini ya kocha Mahili king Kibadeni ambaye aliiongoza timu hiyo
na ikaanza kupata umaarufu mkubwa kutokana na uwezo wa kipesa ambao timu hiyo
ulikuwa nao na kuweza wa kusajili wachezaji toka kila kona hapa nchini na
nje kutokana na mwenendo mzuri wa timu hiyo maji maji ilipata nafasi kuchukua
ubingwa wa muungano mara mbili mfululizo mwaka 1885 hadi 1886.
“Lakini mara baada ya
Gama kuhamishwa miaka ya 1990 timu ilianza kuteteleka ilikuwa chini ya mkuu wa
mkoa mwingine mh Banduka ambaye licha ya kufuata misingi ya Gama kuna kipindi
lilitoka Tamko kuhusu timu hiyo kujiendisha yenyewe ombi ambalo lilishindwa
kukubarika moja kwa moja lakini mkoa wakatoa kibari cha timu kujiendesha
yenyewe na wakasaidia kuipa uwezo wa kufanya Biashara kama kuuza mbolea
pamoja na bia ili kupata pesa ya kuweza kuikwamua timu na mwaka 1995 Banduka
akahamishwa na akaja Mama Anna Makina.
“Makinda aliikuta maji
maji ikiwa imeteteleka ambapo viongozi wa Timu wakamfuata na kumueleza kuhusu
Azimio la Mlale ambalo mzee Gama alilianzisha ambapo Mama Makinda akufumbia
Macho akalipokea kwa mikono miwili na kuanza kulifanyia kazi na akatangaza
kufanya kila kitu kuhusu Maji Maji.
“Kweli Maji Maji
ikasajili wachezaji wazuri na kila mchezaji kutimuziwa maitaji yake yote Ikiwa
ni Pamoja na kuwafungulia akaunti benki na kumwajili kocha ambaye
alimlipa Laki 500,000 kwa mwenzi na akaamlisha kuwa kwa kila mechi ambayo Maji
Maji watacheza mapato ya uwanjani asilimia 70 zitaenda kwa wachezaji wakishinda
,sare asilimia 60 na wakifungwa asilimia 25 ili kuwapa faraja wachezaji na
kutambua kazi yao wawapo uwanjani.
“Uwezo wa Maji Maji
ulipanda gafla ambapo 1996 ikachua nafsi ya 4,mwaka1997 nafasi ya 3 na mwaka
1998 Maji maji ikachukua ubingwa wa muungano kwa mara ya tatu chini ya
wachezaji Bora kabisa hapa nchini.ambapo mwaka huo wachezaji ambao walikuwa
Tishio kwa timu hiyo baadhi yao ni hao wafuatao;-
Shaib Kambanga,David
Mjanja,Omari Kapilima,Godfrey Kikumbizi,Jemes Mwagama,Stevin Mapunda,John
Alex,Kelvin Haule pamoja na Doyi Moke,
“Wengine ni Dello
Ntumba,Omari Hussein,WIlle Martin,Said Msham,Samson Poul, Hamis ngwena pamoja
na Amri Said kikosi ambacho kilikuwa bora hapa nchini kuwai tokea
kwa timu ya maji Maji ambacho ndicho kikawa kikosi cha mwisho cha ushindi.
“Miaka ya 2000 Makinda
akaondoka na akaja mweshimiwa Said Said Kalembo kama mkuu wa mkoa mpya ambaye
akaondoa moja kwa moja Mpango wa kuisaidia timu hiyo kwa asili mia 100 ambapo
akatangaza rasmi kuwa mkoa umefikia kikomo kuendelea kuisaidia Maji Maji
na timu hiyo itaendeshwa na wanachama kama katiba ya timu inavyosema.
“Tamko lile
lilizoofisha sana Maji Maji na wakajaribu kwenda kubembeleza lakini majibu
hayakubadilika pia wakajalibu kufikisha Taarifu kwa mweshimiwa Gama ambaye kwa
kipindi hicho alikuwa mweshimiwa mbunge,lakini gama ilisema kuwa kama mkoa
umekataa kusaidia timu mimi sina la kufanya na uwezo wa kusaidia timu kwa sasa
sina ila ninachokiomba mkateue watu maalum ili kwenda kubembeleza tena kwa mkuu
wa mkoa na akikataa mimi naamini Maji Maji haitakuwepo lazima Itashuka Daraja.
“Maji Maji ilijalibu
kuwatuma wazee kwenda kwa mkuu wa mkoa kubembeleza kwa Mara nyingine napo
Majibu hayakutofautiana na yale ya mwanzo na timu ikawa katika hali Mbaya na
Mwaka 2000 timu ya maji maji ilishuka Daraja lakini Maji Maji wakawa wajanja
wakaipeleka Tff Mahakamani kwa kukiuka sheria.
“kitu ambacho
Kilitokea Maji Maji walishika nafsi ya tatu toka mwisho na toka miaka ya
nyuma timu mbili ndizo ambazo zilikuwa zinashuka Daraja lakini kwa msimu ule
katikati ya ligi TFF wakatangaza kuwa kuanzia mwaka huo timu tatu ndizo zingeshuka
daraja badala ya mbili na mwishoni mwa ligi Maji Maji wakashika nafasi hiyo ya
Tatu hapo ndipo wakaenda maakamani na kuwashitaki TFF kuwa walikosea
badala yake wangetangaza toka mwanzoni mwa ligi na sio katikati ya ligi
Wanalizombe wakashindi kesi hiyo lakini kutokana na kwamba maji maji ilikuwa
katika hali Mbaya Sana ikashuka Daraja Rasmi Mwaka 2001.anahitimisha mzee Ali
Mbalika ambaye alikuwa meneja wa timu ya Maji Maji kwa kipindi hicho.
Lakini kuanzia Mwaka
2003 katibu mkuu wa Sasa wa cha mpira wa miguu manispaa ya Songea Bwana
God Mvula akateuliwa Rasmi kuwa Meneja wa Timu ya Maji Maji nafsi ambayo
anaishikilia hadi hivi sasa, na hapo anaendelea kusimulia Histori ya Maji Maji
kipindi Cha Utawala wake.
“Mwaka 2002 Maji Maji
ikapanda daraja lakini kutotana na timu kuendeshwa kwa mfumo wa kutembeza
Bakuri hali ilikuwa ngumu sana kuendesha timu ambapo mwaka 2005 timu
ikashuka tena hali iliyopelekea kwa timu hiyo kuwa katika mazingira magumu
sana,ambapo baada ya kushuka daraja timu ilipata wasamalia wema ambao walikuwa
ni wanaruvuma waishio Dar,wakafanya usajili wa nguvu na timu ikaweka kambi ya
kudumu Dar lakini mechi zake ilikuwa inachezea kama kawaida Songea na
wakafanikisha kuipandisha timu.
“Lakini Baadae wanacha
wa Maji Maji wakagawanyika na wengi wao wakadai timu irudi Songea hali ambayo
ilisababisha ugomvi mkubwa sana na wale wafadhili wakaachia timu na kumbuka
mwaka 2007 timu ilishuka daraja tena ambapo mechi ya mwisho tulicheza na Kahama
United tukafungwa bao 3-2 kwa kipindi hicho maji maji ilicheza kwa Takribani
mechi Tatu ikiwa na wachezaji saba pekee mara baada ya kutokea mpasuko kati ya
wanachama.
“Mwaka 2008 timu
ikapanda tena daraja mara baada ya kupigana kwa kutumia nguvu kubwa sana na
ikafanya vizuri kwa misimu ya hawali ambapo mwaka 2010 timu ilipata uzamini
toka Caspian ambapo ikapata vifaa vya michezo na pesa za matumizi ndani ya
timu, lakini zikiwa zimesalia mechi Tano ligi kumalizika ulitokea Ugomvi mkubwa
sana kati ya wanachama na uongozi wa timu mimi nikiwa kama meneja wa timu
wanachama walidai kuwa timu ilikuwa inafanya vibaya na ili kuinusuru
wakaichukua na kuiweka mikononi mwao na Sisi Kama viongozi Tukaamua kujiuzulu
na wanachama wakateua uongozi wao.
“uongozi huo ambao
ulifadhiliwa na bwana Super feo,Ottawa pamoja na Mdaula kwa kutoa kiasi kikubwa
cha pesa ili kuinusuru Maji Maji hata hivyo Maji Maji haikuwa na bahati 2011
ikashuka Daraja.
“Baada ya timu kusuka
Daraja na kupoteza kabisa mwelekeo Mimi na Henly Kabela tukaamua kuchukua timu
na kuanza kufanya usajili kwa juhudi zetu na tukaunda uongozi wa mpito kupitia
kwa chama cha soka Manispaa ya Songea [Sufa]ambapo Mwenyekiti alikuwepo Hamis
Gayo,Mkamu Benjamin Mwakasonda, katibu Henily Kabera,Katibu mwenezi Hossam
Hassan Ulaya huku Mimi mwenyewe God Mvula nikaendelea kubakia katika nafasi ya
umeneja,na mwenyekiti wa sasa wa timu Mwana Millanzi alikuwa Mjumbe wa Timu.
“Na tukaanza harakati
za kuinasua timu kupanda daraja ambapo hadi hivi sasa bado tunapambana ili
kuhakikisha timu inasonga mbele kwa kuwa timu imefanya usajili wa kweli baada
ya uongozi wa mpito Kumaliza Muda wake
No comments:
Post a Comment