Na Alex Mwenda-Songea
Klabu ya wanalizombe wa Majimaji ya mjini Songea inatarajia kushika dimbani kucheza mechi ya kirafiki dhidi ya Mbeya city mchezo utakaofanyika katika uwanja wa ccm wilaya Mbinga.
Mchezo huo unatarajia kuanza muda wa saa 10 kamili jioni kwa saa za Afrika mashariki na huenda ukatangazwa moja kwa moja na kituo cha redio mkoani Ruvuma KEYFM 90.5
Mchezo huo ni muhimu kwa timu zote mbili hususani Majimaji ambao wapo katika janga la kushuka daraja msimu huu wa ligi kuu Tanzania bara. Akizungumza na Alex MwendaTZ mjumbe wa kamati ya utendaji ya majimaji Salum Masamaki amedai maandalizi yamekwisha kufanyika na wapo tayari kwa ajili ya mechi.
"Maandalizi yamekamilika ndugu mwandishi na mechi hiyo kwetu ni kipimo tosha kujiandaa na mechi zetu za kanda ya ziwa' amesema Masamaki.
Mara baada ya mechi hii klabu ya Majimaji itasafiri kuelekea Shinyanga kukipiga dhidi ya Mwadui Fc April 7 mwaka huu.
Friday, March 30, 2018
New
MAJIMAJI KUPIMANA NGUVU DHIDI YA MBEYA CITY
About SPORTS ROOM
SoraTemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of SoraTemplates is to provide the best quality blogger templates.
MICHEZO
Labels:
MICHEZO
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment