Simon Msuva (jina lake kamili anaitwa Simon Epigod Msuva ni mchezaji wa kandanda ambaye anacheza nafasi ya winga mshambuliaji katika timu maarufu katika nchi ya Tanzania ambayo ni Young Afrikans.
Msuva ni mfungaji bora wa Ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara kwa msimu wa 2014-2015: alifunga magoli 17. Pia alikuwa mfungaji bora katika Kombe la Mapinduzi lililofanyika mwaka 2015 akifunga magoli 4.
Ana mdogo wake anaitwa James Msuva, nae anacheza katika klabu ya Young Africans. Alisajiliwa kutoka katika akademia ya Simba.
Kuhusu Majaribio
Bwana Msuva amewahi fanyiwa majaribio katika klabu inayoshiriki ligi kuu ya Afrika kusini ambayo ni Bidvest na majaribio hayo akaweza kufanikiwa lakini klabu yake ya Young Africans Sc waligoma kumuuza winga huyu kutokana na makubaliano na timu hio.
No comments:
Post a Comment