Tiketi za Simba na Yanga zaanzwa kuuzwa - ALEX MWENDATZ

Breaking

Saturday, February 11, 2017

Tiketi za Simba na Yanga zaanzwa kuuzwa

Wiki mbili kabla ya pambano la watani wa jadi, Simba na Yanga kuchezwa, tiketi za mtanange huo wa Ligi Kuu tayari zimeanzwa kuuzwa.
Wauzaji wa tiketi hizo, kampuni ya Selcom tayari wameanza kuwatangazia mashabiki kununua tiketi kwa njia ya kadi za kampuni hio.
Image result for SIMBA VS YANGA” Nunua tiketi yako ya mechi kati ya Simba vs  Yanga sasa kuepuka usumbufu. Ongeza salio kwenye Selcom card yako kisha piga *150*50# na chagua Michezo /Burudani. ”
 

Ikumbukwe kuwa katika pambano la kwanza la watani msimu huu mashabiki walipata usumbufu mkubwa wa kununua tiketi kutokana na wengi kununua siku ya mwisho jambo lililopelekea mfumo wa kielektroniki kuzidiwa.

Pambano hilo linalosubiriwa kwa hamu kutokana na timu hizo mbilii kuwa katika vita kali ya kuwania ubingwa na pia kuchagizwa na matokeo ya Oktoba Mosi pale Amissi Tambwe alipofunga bao la utata kabla ya Shiza Kichuya kuisawazishia Simba kwa bao matata, litapigwa tarehe 25 Februari katika dimba la uwanja wa Taifa.

No comments:

Post a Comment