Mchezaji wa KVZ Sultan Juma ambae alifunga bao la pili na la ushindi
katika mchezo wa kombe la Shirikisho barani Afrika KVZ
walipoifunga Messenger Ngozi kutoka Burundi mabao 2-1 mchezo uliochezwa
jana katika uwanja wa Amaan amesema katika mchezo wa marejeano
watapigana kuliko walivyopigana katika mchezo wa jana.
“Leo (Jana) tumepigana na tunashukuru kupata alama 3 nyumbani, sasa
katika mchezo wa pili huko kwao tutapigana kuliko huku ili tulinde
heshma ya Zanzibar,” alisema Sultan.
Nae Ubasenga Danny ambae ni captain wa Messenger Ngozi amekiri wana
kazi kubwa katika mchezo wa marejeano ambapo amesema KVZ si wabaya kama
walivyotegemea.
“Sasa akili yetu yote ni kupindua matokeo haya tulofungwa lakini
tunajua kuwa tuna kazi pevu sana huko nyumbani, ila sina wasi wasi sana
kwa vile ukicheza nyumbani unapata faida fulani, tutawafunga lakini ni
mechi ngumu sana,” alisema Danny.
Wababe hao watarejeana Jumamosi ijayo ya Februari 18, huko mjini Bunjumbura Burundi nyumbani kwa Messenger Ngozi.
Monday, February 13, 2017
New
TUTALINDA HESHIMU BURUNDI KATIKA MCHEZO WA MARUDIANO
About SPORTS ROOM
SoraTemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of SoraTemplates is to provide the best quality blogger templates.
MICHEZO
Labels:
MICHEZO
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment